Zaburi 150

Neno: Kiswahili Contemporary Version

1Msifuni Bwana. Msifuni Mungu katika patakatifu pake, msifuni katika mbingu zake kuu.

2Msifuni kwa matendo yake makuu, msifuni kwa kadiri ya wingi wa ukuu wake.

3Msifuni kwa mvumo wa tarumbeta, msifuni kwa kinubi na zeze,

4msifuni kwa matari na kucheza, msifuni kwa kinanda cha nyuzi na filimbi,

5msifuni kwa matoazi yaliayo, msifuni kwa matoazi yavumayo sana.

6Kila chenye pumzi na kimsifu Bwana. Msifuni Bwana!

Zaburi

Open the interactive reader to switch translations, adjust type, and mark verses — or browse verses by topic.

Neno: Bibilia Takatifu — Kiswahili Contemporary Version. Copyright © 1984, 1989, 2009, 2015 Biblica, Inc. Used under the Biblica Open (Toleo Wazi) License. · Biblica Open License