Zaburi 113

Neno: Kiswahili Contemporary Version

1Msifuni Bwana. Enyi watumishi wa Bwana msifuni, lisifuni jina la Bwana.

2Jina la Bwana na lisifiwe, sasa na hata milele.

3Kuanzia mawio ya jua hadi machweo yake, jina la Bwana linapaswa kusifiwa.

4Bwana ametukuka juu ya mataifa yote, utukufu wake juu ya mbingu.

5Ni nani aliye kama Bwana Mungu wetu, Yeye ambaye ameketi juu kwenye kiti cha enzi,

6ambaye huinama atazame chini aone mbingu na nchi?

7Huwainua maskini kutoka mavumbini, na kuwanyanyua wahitaji kutoka kwenye jalala,

8huwaketisha pamoja na wakuu, pamoja na wakuu wa watu wake.

9Humjalia mwanamke tasa kutulia nyumbani mwake, akiwa mama watoto mwenye furaha. Msifuni Bwana.

Zaburi

Open the interactive reader to switch translations, adjust type, and mark verses — or browse verses by topic.

Neno: Bibilia Takatifu — Kiswahili Contemporary Version. Copyright © 1984, 1989, 2009, 2015 Biblica, Inc. Used under the Biblica Open (Toleo Wazi) License. · Biblica Open License