Zaburi 124

Neno: Kiswahili Contemporary Version

1Kama Bwana asingalikuwa upande wetu; Israeli na aseme sasa:

2kama Bwana asingalikuwa upande wetu, wakati watu walipotushambulia,

3wakati hasira yao ilipowaka dhidi yetu, wangalitumeza tungali hai,

4mafuriko yangalitugharikisha, maji mengi yangalitufunika,

5maji yaendayo kasi yangalituchukua.

6Bwana asifiwe, yeye ambaye hakuruhusu turaruliwe kwa meno yao.

7Tumeponyoka kama ndege kutoka mtego wa mwindaji; mtego umevunjika, nasi tukaokoka.

8Msaada wetu ni katika jina la Bwana, Muumba wa mbingu na dunia.

Zaburi

Open the interactive reader to switch translations, adjust type, and mark verses — or browse verses by topic.

Neno: Bibilia Takatifu — Kiswahili Contemporary Version. Copyright © 1984, 1989, 2009, 2015 Biblica, Inc. Used under the Biblica Open (Toleo Wazi) License. · Biblica Open License