Zaburi 129

Neno: Kiswahili Contemporary Version

1Wamenionea mno tangu ujana wangu; Israeli na aseme sasa:

2wamenionea mno tangu ujana wangu, lakini bado hawajanishinda.

3Wakulima wamelima mgongo wangu, na kufanya mifereji yao mirefu.

4Lakini Bwana ni mwenye haki; amenifungua toka kamba za waovu.

5Wale wote waichukiao Sayuni na warudishwe nyuma kwa aibu.

6Wawe kama majani juu ya paa, ambayo hunyauka kabla hayajakua;

7kwa hayo mvunaji hawezi kujaza vitanga vyake, wala akusanyaye kujaza mikono yake.

8Wale wapitao karibu na wasiseme, “Baraka ya Bwana iwe juu yako; tunakubariki katika jina la Bwana.”

Zaburi

Open the interactive reader to switch translations, adjust type, and mark verses — or browse verses by topic.

Neno: Bibilia Takatifu — Kiswahili Contemporary Version. Copyright © 1984, 1989, 2009, 2015 Biblica, Inc. Used under the Biblica Open (Toleo Wazi) License. · Biblica Open License