Zaburi 130

Neno: Kiswahili Contemporary Version

1Kutoka vilindini ninakulilia, Ee Bwana.

2Ee Bwana, sikia sauti yangu. Masikio yako na yawe masikivu kwa kilio changu unihurumie.

3Kama wewe, Ee Bwana, ungeweka kumbukumbu ya dhambi, Ee Bwana, ni nani angeliweza kusimama?

4Lakini kwako kuna msamaha, kwa hiyo wewe unaogopwa.

5Namngojea Bwana, nafsi yangu inangojea, katika neno lake naweka tumaini langu.

6Nafsi yangu inamngojea Bwana kuliko walinzi waingojeavyo asubuhi, naam, kuliko walinzi waingojeavyo asubuhi.

7Ee Israeli, mtumaini Bwana, maana kwa Bwana kuna upendo usiokoma, na kwake kuna ukombozi kamili.

8Yeye mwenyewe ataikomboa Israeli kutoka dhambi zao zote.

Zaburi

Open the interactive reader to switch translations, adjust type, and mark verses — or browse verses by topic.

Neno: Bibilia Takatifu — Kiswahili Contemporary Version. Copyright © 1984, 1989, 2009, 2015 Biblica, Inc. Used under the Biblica Open (Toleo Wazi) License. · Biblica Open License