Zaburi 121

Neno: Kiswahili Contemporary Version

1Nayainua macho yangu nitazame vilima, msaada wangu utatoka wapi?

2Msaada wangu hutoka kwa Bwana, Muumba wa mbingu na dunia.

3Hatauacha mguu wako uteleze, yeye akulindaye hatasinzia,

4hakika, yeye alindaye Israeli hatasinzia wala hatalala usingizi.

5Bwana anakulinda, Bwana ni uvuli wako mkono wako wa kuume,

6jua halitakudhuru mchana, wala mwezi wakati wa usiku.

7Bwana atakukinga na madhara yote, atayalinda maisha yako,

8Bwana atakulinda unapoingia na unapotoka, tangu sasa na hata milele.

Zaburi

Open the interactive reader to switch translations, adjust type, and mark verses — or browse verses by topic.

Neno: Bibilia Takatifu — Kiswahili Contemporary Version. Copyright © 1984, 1989, 2009, 2015 Biblica, Inc. Used under the Biblica Open (Toleo Wazi) License. · Biblica Open License