Ezra 2

Neno: Kiswahili Contemporary Version

1Basi hawa ndio watu wa jimbo waliotoka uhamishoni, ambao Nebukadneza mfalme wa Babeli alikuwa amewachukua mateka hadi Babeli (walirudi Yerusalemu na Yuda, kila mmoja kwenye mji wake,

2wakiwa wamefuatana na Zerubabeli, Yeshua, Nehemia, Seraya, Reelaya, Mordekai, Bilshani, Mispari, Bigwai, Rehumu na Baana): Orodha ya wanaume kati ya watu wa Israeli ilikuwa:

3wazao wa Paroshi 2,172

4wazao wa Shefatia 372

5wazao wa Ara 775

6wazao wa Pahath-Moabu (wa jamaa ya Yeshua na Yoabu) 2,812

7wazao wa Elamu 1,254

8wazao wa Zatu 945

9wazao wa Zakai 760

10wazao wa Bani 642

11wazao wa Bebai 623

12wazao wa Azgadi 1,222

13wazao wa Adonikamu 666

14wazao wa Bigwai 2,056

15wazao wa Adini 454

16wazao wa Ateri (kupitia Hezekia) 98

17wazao wa Besai 323

18wazao wa Yora 112

19wazao wa Hashumu 223

20wazao wa Gibari 95

21watu wa Bethlehemu 123

22watu wa Netofa 56

23watu wa Anathothi 128

24watu wa Azmawethi 42

25wazao wa Kiriath-Yearimu, Kefira na Beerothi 743

26wazao wa Rama na Geba 621

27watu wa Mikmashi 122

28watu wa Betheli na Ai 223

29wazao wa Nebo 52

30wazao wa Magbishi 156

31wazao wa Elamu ile ingine 1,254

32wazao wa Harimu 320

33wazao wa Lodi, Hadidi na Ono 725

34wazao wa Yeriko 345

35wazao wa Senaa 3,630

36Makuhani: wazao wa Yedaya (kwa jamaa ya Yeshua) 973

37wazao wa Imeri 1,052

38wazao wa Pashuri 1,247

39wazao wa Harimu 1,017

40Walawi: wazao wa Yeshua na Kadmieli (kupitia jamaa ya Hodavia) 74

41Waimbaji: wazao wa Asafu 128

42Mabawabu wa lango la Hekalu: wazao wa Shalumu, Ateri, Talmoni, Akubu, Hatita na Shobai 139

43Watumishi wa Hekalu: wazao wa Siha, Hasufa, Tabaothi,

44wazao wa Kerosi, Siaha, Padoni,

45wazao wa Lebana, Hagaba, Akubu,

46wazao wa Hagabu, Shalmai, Hanani,

47wazao wa Gideli, Gahari, Reaya,

48wazao wa Resini, Nekoda, Gazamu,

49wazao wa Uza, Pasea, Besai,

50wazao wa Asna, Meunimu, Nefusimu,

51wazao wa Bakbuki, Hakufa, Harhuri,

52wazao wa Basluthi, Mehida, Harsha,

53wazao wa Barkosi, Sisera, Tema,

54wazao wa Nesia na Hatifa.

55Wazao wa watumishi wa Solomoni: wazao wa Sotai, Hasaferethi, Peruda,

56wazao wa Yaala, Darkoni, Gideli,

57wazao wa Shefatia, Hatili, Pokereth-Hasebaimu na Ami.

58Watumishi wa Hekalu wote na wazao wa watumishi wa Solomoni 392

59Wafuatao walikuja kutoka miji ya Tel-Mela, Tel-Harsha, Kerubu, Adoni na Imeri, lakini hawakuweza kuthibitisha kwamba jamaa zao zilikuwa uzao wa Israeli:

60wazao wa Delaya, Tobia na Nekoda 652

61Kutoka miongoni mwa makuhani: Wazao wa Hobaya, Hakosi, Barzilai (mtu aliyekuwa amemwoa binti wa Barzilai, Mgileadi, naye akaitwa kwa jina hilo).

62Hawa walitafuta orodha za jamaa zao, lakini hawakuonekana humo, kwa hiyo waliondolewa kutoka kundi la makuhani kwa kuwa walihesabiwa kuwa najisi.

63Mtawala aliagiza kuwa wasile chochote miongoni mwa vyakula vitakatifu hadi kuwe kuhani atakayehudumu kwa Urimu na Thumimu.

64Jumla ya watu wote waliorudi walikuwa 42,360;

65tena zaidi ya hao walikuwepo watumishi wa kiume na wa kike 7,337; pia walikuwamo waimbaji wanaume na wanawake 200.

66Walikuwa na farasi 736, nyumbu 245,

67ngamia 435 na punda 6,720.

68Walipofika kwenye nyumba ya Bwana huko Yerusalemu, baadhi ya viongozi wa jamaa walitoa sadaka za hiari kwa ajili ya kujenga upya nyumba ya Mungu katika eneo lake.

69Wakatoa kwa kadiri ya uwezo wao na kutia katika hazina darkoni 61,000 za dhahabu, mane 5,000 za fedha, na mavazi 100 ya ukuhani kwa ajili ya kazi hiyo.

70Makuhani, Walawi, waimbaji, mabawabu, na watumishi wa Hekalu waliishi katika miji yao wenyewe, pamoja na baadhi ya watu wengine, nao Waisraeli waliosalia waliishi katika miji yao.

Ezra

Open the interactive reader to switch translations, adjust type, and mark verses — or browse verses by topic.

Neno: Bibilia Takatifu — Kiswahili Contemporary Version. Copyright © 1984, 1989, 2009, 2015 Biblica, Inc. Used under the Biblica Open (Toleo Wazi) License. · Biblica Open License